Podcasts by Category

Haki ya Mungu Inayofunuliwa Katika Kitabu cha Warumi - BWANA Wetu Aliyefanyika Kuwa Haki ya Mungu (II)

Haki ya Mungu Inayofunuliwa Katika Kitabu cha Warumi - BWANA Wetu Aliyefanyika Kuwa Haki ya Mungu (II)

The New Life Mission

Haki ya Mungu ipo wazi na ni tofauti kabisa na haki za wanadamu. Haki ya Mungu imefunuliwa katika injili ya maji na Roho ambayo ilitimizwa kwa ubatizo wa Yesu toka kwa Yohana na damu yake Msalabani. Tunapaswa kurudi katika imani inayoamini katika haki ya Mungu kabla hatujachelewa. Je, unafahamu ni kwa nini ilimpasa Yesu kubatizwa na Yohana Mbatizaji? Ikiwa Yohana asingelimbatiza Yesu, basi dhambi zetu zingekuwa hazikupitishwa kwa Yesu. Yohana Mbatizaji alikuwa ndiye mkuu kuliko wanadamu wote, na ule ubatizo ambao alimpatia Yesu ulikuwa ni sharti muhimu la Mungu ili kuweza kuzipitisha dhambi zetu toka kwetu kwenda kwa Yesu. Yesu alibatizwa ili kuzibeba dhambi zote za ulimwengu katika mabega yake, kisha aliimwaga damu yake Msalabani ili kulipa mshahara wa dhambi hizo zote. Mambo haya yote yamebadilisha kikamilifu uelewa wangu wa zamani juu ya kuzaliwa tena upya wakati nilipokuwa nikifahamu juu ya damu ya Msalaba tu. Kwa sasa Mungu ametufundisha juu ya haki ya Mungu jinsi ilivyo ili kwamba tuweze kufahamu na kuamini kikamilifu katika haki yake. Ninamshukuru Bwana kwa baraka hizi zote. https://www.bjnewlife.org/ https://youtube.com/@TheNewLifeMission https://www.facebook.com/shin.john.35

30 - SURA YA 7-1. Utangulizi Kwa Sura ya 7
0:00 / 0:00
1x
  • 30 - SURA YA 7-1. Utangulizi Kwa Sura ya 7

    Kwa kuutambua ukweli kuwa kabla ya ukombozi wake mwili wake ulikuwa umehukumiwa kifo na Sheria ya Mungu, basi ndio maana Mtume Paulo alilifanya ungamo lake kwa kuamini kuwa alikuwa ameifia dhambi katika Yesu Kristo. Kabla hatujakutana na haki ya Mungu—yaani kabla hatujazaliwa upya—sisi ambao tunamwamini Kristo tulizoea kuishi chini ya himaya na laana ya Sheria. Hivyo, ikiwa tusingekutana na Yesu ambaye ametuletea haki ya Mungu basi Sheria ingeendelea kututawala. https://www.bjnewlife.org/https://youtube.com/@TheNewLifeMissionhttps://www.facebook.com/shin.john.35

    Fri, 13 Jan 2023 - 18min
  • 29 - SURA YA 7-2. Kiini cha Imani ya Paulo: Ungana na Kristo Baada ya Kuifia Dhambi (Warumi 7:1-4)

    Je, umewahi kuona bunda la nyuzi zilizojisokota? Ikiwa unajaribu kuifahamu sura hii pasipo kuufahamu ukweli wa ubatizo wa Yesu ambao Mtume Paulo aliuamini, basi ni hakika kuwa imani yako itakuwa katika wakati mgumu kuliko hapo kabla. https://www.bjnewlife.org/https://youtube.com/@TheNewLifeMissionhttps://www.facebook.com/shin.john.35

    Fri, 13 Jan 2023 - 49min
  • 28 - SURA YA 7-3. Sababu Inayotufanya Tumsifu Bwana (Warumi 7:5-13)

    Ninamsifu Bwana ambaye ameniongoza hadi kuonana na ninyi watu wa Mungu kwa mara nyingine tena. Kwa kweli ninamshukuru sana Mungu kwa kunibariki na kunifanya niishi maisha yenye furaha hadi leo hii. Mungu ameendelea kuwa pamoja nami na amekuwa akinihurumia ingawa kulikuwa na nyakati ambazo nilikuwa najisikia kukatishwa tamaa, nyakati ambazo nilikutana na magumu na kupata udhaifu ndani yangu katika vipindi mbalimbali. Mungu amekuwa makini na amekuwa upande wangu katika maisha yangu yote katika shida na katika furaha. Hakukuwa na wakati wowote ambapo Mungu aliniacha hata kwa sekunde moja. https://www.bjnewlife.org/https://youtube.com/@TheNewLifeMissionhttps://www.facebook.com/shin.john.35

    Fri, 13 Jan 2023 - 29min
  • 27 - SURA YA 7-4. Miili Yetu Ambayo Inautumikia Mwili Tu (Warumi 7:14-25)

    Sisi hatuwezi kufanya jambo lolote ikiwa Mungu hatendi kazi akiwa upande wetu. Mungu wetu anatutunza na anatusaidia. Hebu tuliangalie Neno la Mungu. Warumi 7:14-25 inatueleza sisi kuwa Mtume Paulo alijiona yeye mwenyewe kuwa anaishi katika mwili hali akiwa ameuzwa chini ya dhambi. Pia aligundua kuwa kwa sababu ya sheria mwili hauwezi kufanya lolote zaidi ya kuendelea kufanya dhambi muda wote atakapokuwa hai. https://www.bjnewlife.org/https://youtube.com/@TheNewLifeMissionhttps://www.facebook.com/shin.john.35

    Fri, 13 Jan 2023 - 32min
  • 26 - SURA YA 7-5. Mwili Unaitumikia Sheria ya Dhambi (Warumi 7:24-25)

    Biblia inatueleza sisi pia kuwa, “kwa akili zangu naitumikia sheria ya Mungu, bali kwa mwili wangu sheria ya dhambi.” Na hizo ndio sheria zinazotutawala. Mioyo yetu imeumbwa kumpenda Mungu na kuupenda ukweli, lakini ni kawaida kwa mwili kuitumikia sheria ya dhambi. Neno la Mungu linatueleza sisi kuwa moyo unaitumikia injili na haki ya Mungu ilhali mwili unaitumikia dhambi tu. https://www.bjnewlife.org/https://youtube.com/@TheNewLifeMissionhttps://www.facebook.com/shin.john.35

    Fri, 13 Jan 2023 - 38min
Show More Episodes